Mshambuliaji wa Brazil Neymar ,30, anafikiri kuondoka katika
klabu yake ya PSG mwisho wa msimu huu baada ya kugundua kwamba klabu hiyo iko
tayari kwa mshambuliaji huyo kuondoka , huku ajenti wake akiwasiliana na
Chelsea kuona iwapo wana hamu ya kumsajili. (ESPN)
Manchester United inakaribia kumsajili kiungo wa Denmark Christian Eriksen baada ya kandarasi yake katika klabu ya Brentford kuisha (Star)
Chelsea, Paris St-Germain na Bayern Munich wanapigania kumsajili mshambuliaji wa Barcelona na Ufaransa Ousmane Dembele, huku mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 25 akipatikana kwa uhamisho wa bila malipo (Marca)